• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Anuani za watumishi |
Mpimbwe District Council
Mpimbwe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Maji
      • Ardhi na Mali asili
      • Kilimo , Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kazi na zima Moto
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mazingira na usafi
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • sheria
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • ufugaji wa nyuki
      • TEHAMA na Habari
      • Ugavi na ununuzi
    • Sehemu
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
  • Machapisho
    • Muongozo
    • Hatua
    • Taarifa
    • Sheria
      • sheria ndogo
    • Fomu ya Maombi
      • Mkataba
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Albamu ya Picha
    • Video
    • Mpya
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Matukio
    • Hotuba
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyopangwa

DC SANGA ASISITIZA WANANCHI WA MLELE KUWAPELEKA WATOTO SHULE IFIKAPO JANUARY, 2023.

Posted on: October 25th, 2022

Akizungumza na wadau wa maendeleo katika ukumbi wa shule ya msingi Majimoto halmashauri ya wilaya ya Mpimbwe Mkoa wa Katavi Mhe. Sanga amesema serikali ya awamu ya sita chini ya usimamizi wa Mhe. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeendelea kutoa huduma kwa jamii yake katika nyanja zote imiwemo afya, elimu, miundombinu ya barabara, umeme, maji  na kutekeleza miradi mingine katika halmashauri ya wilaya ya Mpimbwe.


Akifafanua umuhimu wa watoto kupatiwa nafasi ya kujiendeleza kielimu, Mhe Sanga amewataka wananchi hao kuwaandikisha wototo waliofikia umri wa kuanza darasa la awali huku wakizingatia umri sahihi wa watoto hao ili wapate msingi mzuri wa elimu kabla ya kuanza masomo ya darasa la kwanza kuliko kuwaacha nyumbani.


"Ninawaomba wazazi tuwe na mwamko wa elimu katika maeneo yenu, tuwapeleke watoto wetu wakapate elimu ya awali kabla ya kuanza masomo ya darasa la kwanza, kuliko kuwaacha majumbani mwetu wakitusaidia shughuli za familia hii haitatusaidia kuokoa kizazi hiki" Amesema Mhe. Sanga


Mhe. Sanga amewaomba wazazi wa wanafunzi waliohitimu darasa la saba mwaka huu 2022 kuacha tabia ya kuwaachisha wanafunzi shule hasa kwa wale wanaotarajiwa kuanza masomo yao ya kidato cha kwanza januari 2023 kwa sababu mbalimbali ikiwemo kuwaozesha.


"Tutachukua hatua kali za kinidhamu kwa wazazi ambao kwa namna moja ama nyingine watakwamisha mwanafunzi kujiunga kidato cha kwanza 2023, ninazema haya kwa uchungu mkubwa nikiwa kama mzazi kwani kuna tabia za wazazi wasio na uchungu kwa watoto wao huwaozesha mapema ili kupata mali, ninalaani tabia na isitokee" Amesema Mhe. Sanga


"Matarajio ya rais wetu Mhe. Samia Suluhu Hassan ni kuona watoto wanaohitimu darasa la saba na kufaulu mtihani wao wote wanaingia kidato cha kwanza pasipo kupata kikwazo cha aina yoyote, na ndiyo maana serikali kuu kwa mwaka huu imetupatia kiasi cha zaidi ya shilingi Bilioni 1.3 ili tuzisimamie kuhakikisha tunajenga vyumba vya madarasa ambayo watoto hawa watayatumia ifikapo 2023" Amesema Mhe. Sanga


Mhe. Sanga amewataka wananchi pia kujenga vyoo bora katika maeneo yao ili kuepuka magonjwa ya milipuko kama kipindupindu  ambacho husababishwa na uchafu wa mazingira.


"Ndugu zangu wadau wa maendeleo ninawaomba tukaisaidie jamii kila mtu kwa nafasi yake kutoa elimu juu ya kuwa na vyoo bora na si bora choo katika makazi yetu, lakini kuepuka kushikana mikono ili kuepukana na magonjwa mbalimbali ikiwepo ugonjwa wa Ebora. Amesema Mhe. Sanga


Katika hatua nyingine  Mkuu huyo wa wilaya amewataka wananchi kuzingatia kanuni na taratibu za maswala ya lishe bora kwa jamii.


"Mpimbwe ni eneo ambalo linajitahidi kwa kulima mazao lakini  wananchi hawazingatii kupata chakula bora, ulaji wa nyakula vilivyo poa au kula chakula kilicholala kikiwa cha baridi si afya bora kwa watoto wetu kwa sababu kuna uwezekano mkubwa kwa watoto hao kupata matatizo ya utapia mlo, hivyo tujitahidi kurinda afya za watoto.


kwa upande wake mkurungenzi mtendaji  wa halmashauri ya  wilaya ya Mpimbwe Bi. Catherine Mashalla amewasainisha mikataba watendaji wa vijiji na kata katika wilaya yake ili wakasimamie shughuli za masuala ya lishe mbele ya mkuu wa wilaya hiyo Mhe. Sanga.


Ikumbukwe kuwa Wilaya ya Mlele ina halmashauri mbili ambazo ni halmashauri ya wilaya ya Mlele na halmashauri ya wilaya ya Mpimbwe, Mwaka 2021 halmashauri za wilaya ya Mpimbwe na Mlele zilipokea kiasi cha zaidi ya shilingi bilioni 3.3 kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo ya elimu.


Aidha serikali ilitoa fedha kwa halmashauri hizo mbili kiasi cha zaidi ya shilingi Bilioni 4.3 kwa ajili kutekeleza miradi ya maenedeleo ya Afya, kiasi cha zaidi shilingi  Bilioni 3.1 ilielekezwa kutekeleza miradi ya Maji wilayani hapo.


Mhe. Sanga amefafanua kuwa kwa kipindi cha mwaka 2022/2023 halmashauri hizo zimepokea pia kiasi cha zaidi ya shilingi milioni 937,977,000.00 ikiwa ni kwa ajili ya kutoa huduma ya umeme kwa jamii, pia kiasi cha zaidi ya Bilioni 5.2 kwa ajili ya miundombinu ya barabara.



MWISHO.


*Imetolewa na:*

Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini.

*Halmashuri ya Wilaya ya Mpimbwe.*

Matangazo

  • BOFYA HAPA KUONA ORODHA YA WANAFUNZI WALIOPANGWA KWENDA SHULE MOJA December 20, 2023
  • TANGAZO LA KAZI YA KUJITOLEA February 15, 2024
  • Tangazo la Nafasi za Kazi September 17, 2019
  • Tangazo la nafasi za Kazi za Muda April 21, 2020
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • MPANGO WA MATUMIZI YA ARDHI HALMASHAURI YA WILAYA YA MPIMBWE

    April 05, 2025
  • MKURUGENZI MTENDAJI WA H/W YA MPIMBWE AZINDUA MAFUNZO YA UWEZESHAJI WANAWAKE KIUCHUMI KWA WATENDAJI WA KATA NA VIJIJI

    February 12, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LA MPIMBWE LAWEKA MIKAKATI YA KUBORESHA LISHE NA MIRADI YA MAENDELEO

    February 11, 2025
  • Uandikishaji kwenye Daftari la Wapiga kura

    October 11, 2024
  • Angalia yote

Video

Vivutio Vya Watali katika Hifadhi ya Taifa Katavi
Video Zaidi

Kiungo cha Haraka

  • Chuo kikiku cha kilimo Sua cha tembelea Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe kwa ajili ya uanzishaji wa chuo cha kilimo Ndani ya Mkoa wa Katavi
  • Mpimbwe A Conservation and Development Project
  • Revenue collection dashboard for Katavi Region
  • Mkoa wa katavi

Kurasa za Karibu

  • NECTA
  • UTUMISHI
  • WIZARA YA ELIMU, SAYANSI, TEKNOLOJIA NA MAFUNZO YA UFUNDI
  • OR-TAMISEMI
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya wilaya ya Mpimbwe- Usevya

    Sanduku la Posta: 245

    Telephone: 0625732265

    Mobile: 0625732265

    Barua Pepe: ded@mpimbwedc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Mpimbwe. Haki zote zimehifadhiwa