• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Anuani za watumishi |
Mpimbwe District Council
Mpimbwe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Maji
      • Ardhi na Mali asili
      • Kilimo , Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kazi na zima Moto
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mazingira na usafi
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • sheria
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • ufugaji wa nyuki
      • TEHAMA na Habari
      • Ugavi na ununuzi
    • Sehemu
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
  • Machapisho
    • Muongozo
    • Hatua
    • Taarifa
    • Sheria
      • sheria ndogo
    • Fomu ya Maombi
      • Mkataba
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Albamu ya Picha
    • Video
    • Mpya
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Matukio
    • Hotuba
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyopangwa

kilimo cha umwagiliaji kitasaidia katika kuinua Uchumi wa Mkulima .

Posted on: May 10th, 2022

Naibu Waziri wa kilimo Anthony Mavunde amefanya ziara katika Halmashauri ya wilaya ya Mpimbwe Mkoa wa Katavi , ambapo ametembelea Skimu ya umwagiliaji katika kijiji cha kilida kata ya Mamba  na kugawa matrekta ya Mkono yaani Powertillers kwa wakulima waliokopeshwa  na Kampuni ya ZANA BORA kupitia Benk ya NMB.

 Akisoma Taarifa   Ndugu  George  Magile Mkuu wa Idara ya kilimo amesema Katika kuhakikisha  Wakulima wanapata huduma bora Halmashauri imeweka mkakati wa kuboresha huduma za ugani kwa kuhamasisha wakulima wajiunge katika  vikundi iliwaweze kufikiwa  kwa urahisi na mpaka sasa vikundi 59  vimeanzishwa  katika kata  mbalimbali  za Halmashauri yaWilaya ya  Mpimbwe.

Jumla ya Wakulima 2134 wamepata mafunzo ya uhifadhi  nafaka salama na wa wakulima 1937 wamepata mafunzo ya kilimo bora  cha mbongamboga  na Matunda .

Aidha wakulima wamepata elimu juu  ya matumizi sahihi na salama ya viuatilifu  na matumizi sahihi  ya mbolea na mbegu bora, kuboreshwa  miundombinu ya Kilimo kwa kukarabati  na kujenga  mifereji ya umwagiliaji kwa lengo la kupunguza  upotevu wa maji,  jumla ya Km3.5 za Mifereji zimeboreshwa  kienyeji pia jumla ya km 59 za barabara  zimekarabatiwa ili kurahisisha usafirishaji wa mazao ya wakulima.

Ndg. Magile amesema katika Halmashauri ya Mpimbwe   Maghala ya kuhifadhia mazao 10 yaliyojengwa na Serikali  yanatumika  na Maghala 147 ya watu binafsi yanatumika  kuhifadhia  mazao ya Wakulima.

Aidha Wakulima katika  msimu huu wa kilimo  toka vyama vya msingi AMCOS wameweza kukopeshwa fedha na pembejeo  za kilimo zenye  jumla ya Tsh 2,074,480,000

Jumla ya wakulima 53 wamepata   Trekta za mkono yani powertillers zenye thamani ya TSh. 683,700,000

Kwa upande wake Mbunge wa jimbo la Kavuu Mh. Geofrey Pinda ameishukuru kampuni ya ZANA BORA kwa kushirikana na Benki ya NMB kwa kutoa zana hizo zitakazo saidia wakulima katika kuzalisha  mazao.

Naibu waziri wa kilimo Mh.Anthony Mavunde  amesema “bonde Hili  ni muhimu kwa nchi yetu ya Tanzania  hasa katika uzalishaji wa mazao  mnaoufanya hapa, ndio maana sisi kama Wizara Tunaliangalia bonde hili kwa jicho la tofauti tukiweka nguvu hapa tutaisaidia Tanzania na siyo Mkoa wa  Katavi  peke yake”

Mh .Mavunde amesema katika malengo ambayo Serikali imejiwekea nikuwa na uzalishaji mkubwa wa Mazao hasa ya  nafaka   kufikia ziada ya  kuuza Nje ya nchi,   ili kuweza kufikia malengo hayo tusilime kilimo cha kutengemea mvua peke yake badala yake tujikite katika skimu za umwagiliaji.

Aidha Mh. Mavunde amesisitiza kuendelea kutumia Teknolojia za kisasa ili kuweza kuacha kulima kwa kutumia jembe la mkono na badala yake kutumia Trekta.

 Na Odetha Salum

Matangazo

  • BOFYA HAPA KUONA ORODHA YA WANAFUNZI WALIOPANGWA KWENDA SHULE MOJA December 20, 2023
  • TANGAZO LA KAZI YA KUJITOLEA February 15, 2024
  • Tangazo la Nafasi za Kazi September 17, 2019
  • Tangazo la nafasi za Kazi za Muda April 21, 2020
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • MPANGO WA MATUMIZI YA ARDHI HALMASHAURI YA WILAYA YA MPIMBWE

    April 05, 2025
  • MKURUGENZI MTENDAJI WA H/W YA MPIMBWE AZINDUA MAFUNZO YA UWEZESHAJI WANAWAKE KIUCHUMI KWA WATENDAJI WA KATA NA VIJIJI

    February 12, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LA MPIMBWE LAWEKA MIKAKATI YA KUBORESHA LISHE NA MIRADI YA MAENDELEO

    February 11, 2025
  • Uandikishaji kwenye Daftari la Wapiga kura

    October 11, 2024
  • Angalia yote

Video

Vivutio Vya Watali katika Hifadhi ya Taifa Katavi
Video Zaidi

Kiungo cha Haraka

  • Chuo kikiku cha kilimo Sua cha tembelea Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe kwa ajili ya uanzishaji wa chuo cha kilimo Ndani ya Mkoa wa Katavi
  • Mpimbwe A Conservation and Development Project
  • Revenue collection dashboard for Katavi Region
  • Mkoa wa katavi

Kurasa za Karibu

  • NECTA
  • UTUMISHI
  • WIZARA YA ELIMU, SAYANSI, TEKNOLOJIA NA MAFUNZO YA UFUNDI
  • OR-TAMISEMI
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya wilaya ya Mpimbwe- Usevya

    Sanduku la Posta: 245

    Telephone: 0625732265

    Mobile: 0625732265

    Barua Pepe: ded@mpimbwedc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Mpimbwe. Haki zote zimehifadhiwa