• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Anuani za watumishi |
Mpimbwe District Council
Mpimbwe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Maji
      • Ardhi na Mali asili
      • Kilimo , Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kazi na zima Moto
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mazingira na usafi
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • sheria
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • ufugaji wa nyuki
      • TEHAMA na Habari
      • Ugavi na ununuzi
    • Sehemu
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
  • Machapisho
    • Muongozo
    • Hatua
    • Taarifa
    • Sheria
      • sheria ndogo
    • Fomu ya Maombi
      • Mkataba
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Albamu ya Picha
    • Video
    • Mpya
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Matukio
    • Hotuba
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyopangwa

MPANGO WA MATUMIZI YA ARDHI HALMASHAURI YA WILAYA YA MPIMBWE

Posted on: April 5th, 2025

Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe, leo tarehe 4 Aprili 2025, imepokea timu ya wataalamu kutoka Tume ya Taifa ya Ardhi kwa lengo la kutoa elimu kwa wananchi kuhusu matumizi bora ya ardhi. Mafunzo hayo yametolewa kwa wajumbe wa vijiji, vitongoji pamoja na wananchi wa maeneo mbalimbali ya Mpimbwe, ikiwemo kijiji cha Chamalendi, kijiji cha Kashishi, Minyoso, Mirumba, Ikuba, Nyambwe, Mkwajuni, Msadya na mengineyo. Lengo kuu ni kuwafikishia wananchi elimu itakayosaidia kutatua migogoro ya ardhi, pamoja na kuwawezesha kupata hati miliki za maeneo yao kisheria. Wataalamu hao wameambatana na Mkuu wa Kanda wa Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi, Ndugu Emmanuel Magembe, ambaye ameongoza mafunzo hayo kwa kuzingatia umuhimu wa elimu hii katika usimamizi bora wa ardhi na kutatua changamoto zinazojitokeza katika maeneo haya.


Katika mafunzo hayo, wataalamu wameeleza kwa kina malengo ya mpango wa matumizi bora ya ardhi ikiwa ni pamoja na kuwezesha usimamizi mzuri wa ardhi, kuhamasisha uzalishaji wenye tija, na kuhakikisha upatikanaji wa rasilimali za ardhi kwa haki na usawa. Elimu hiyo imetoa msisitizo kwa wananchi kutumia ardhi kwa kuzingatia mipango iliyowekwa ili kuongeza thamani ya ardhi na kuchochea maendeleo katika jamii.


Aidha, wataalamu hao wameeleza kuwa mpango wa matumizi bora ya ardhi una faida nyingi kwa jamii, ikiwemo kuondoa migogoro ya ardhi baina ya watumiaji, kusaidia utunzaji wa vyanzo vya maji, kuzuia ufyekaji wa misitu na mapori yaliyohifadhiwa kwa matumizi maalum, pamoja na kuwezesha matumizi endelevu ya ardhi. Wananchi wamehamasishwa kushiriki kikamilifu katika utekelezaji wa mpango huu kwa manufaa ya sasa na vizazi vijavyo.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili October 12, 2025
  • Tangazo la Nafasi za Kazi September 17, 2019
  • Tangazo la nafasi za Kazi za Muda April 21, 2020
  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili wa Ajira za muda Katika Mfumo wa anwani za Makazi March 15, 2022
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • Shamrashamra za Wananchi wa Jimbo la Kavuu kujiandaa kumpokea Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

    October 15, 2025
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili

    October 12, 2025
  • MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU HALMASHAULI YA WILAYA YA MPIMBWE

    September 27, 2025
  • Tangazo la Utoaji wa Fomu za Uteuzi kwa wagombea wa Ubunge na Udiwani kwa Jimbo la Kavuu

    August 14, 2025
  • Angalia yote

Video

Vivutio Vya Watali katika Hifadhi ya Taifa Katavi
Video Zaidi

Kiungo cha Haraka

  • Chuo kikiku cha kilimo Sua cha tembelea Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe kwa ajili ya uanzishaji wa chuo cha kilimo Ndani ya Mkoa wa Katavi
  • Mpimbwe A Conservation and Development Project
  • Revenue collection dashboard for Katavi Region
  • Mkoa wa katavi

Kurasa za Karibu

  • NECTA
  • UTUMISHI
  • WIZARA YA ELIMU, SAYANSI, TEKNOLOJIA NA MAFUNZO YA UFUNDI
  • OR-TAMISEMI
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya wilaya ya Mpimbwe- Usevya

    Sanduku la Posta: 245

    Telephone: 0625732265

    Mobile: 0625732265

    Barua Pepe: ded@mpimbwedc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Mpimbwe. Haki zote zimehifadhiwa