• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Anuani za watumishi |
Mpimbwe District Council
Mpimbwe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Maji
      • Ardhi na Mali asili
      • Kilimo , Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kazi na zima Moto
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mazingira na usafi
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • sheria
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • ufugaji wa nyuki
      • TEHAMA na Habari
      • Ugavi na ununuzi
    • Sehemu
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
  • Machapisho
    • Muongozo
    • Hatua
    • Taarifa
    • Sheria
      • sheria ndogo
    • Fomu ya Maombi
      • Mkataba
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Albamu ya Picha
    • Video
    • Mpya
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Matukio
    • Hotuba
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyopangwa

BARAZA LA MADIWANI HALMASHURI YA URAMBO LAJIFUNZA UFUGAJI WA NYUKI HALMASHAURI YA MPIMBWE MKOA WA KATAVI.

Posted on: November 15th, 2022

*15.11.2022*



*TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI



Baraza la Madiwani la Halmshauri ya wilaya ya Urambo Mkoa wa Tabora  wakiambatana na wakuu wa Idara kutoka halmashauri hiyo wamefanya ziara ya mafunzo ya kufuga na kuhifadhi nyuki.



Wakiambatana na Mwenyekiti wa Halmashuri ya Mpimbwe Sailas Irumba , Mkurungenzi mtendaji wa Halmashuri ya wilaya ya  Mpimbwe  Bi. Catherine Mashalla,  Waheshimiwa  Madiwani wa Halmashauri ya Mpimbwe na baadhi ya Wakuu wa Idara, wametembelea katika chanzo cha chemichemi ya inayotoa maji yamoto  kilichopo katika kijiji cha Majimoto ambacho hutoa maji yake ya moto ambayo ni asili, Pia wametembelea katika Chuo Kikuu  cha Sokoine  Tawi la Mizengo Pinda ambacho kipo katika  Halmashuri  ya Wilaya ya Mpimbwe kwa ajili ya kupata mafunzo ya ufugaji wa nyuki kwa kina .



Akitoa mafunzo ya namna ya kufuga nyuki pamoja na faida zake, Mhadhiri wa Chuo hicho Evaristus Magani amesema kuwa ufugaji wa kisasa unasaidia sana katika kuhakikisha  upatikanaji wa asali na Nta unakuwa kwa wingi licha ya kuwa nyuki  huzalisha mazao mengi ambayo watu hawajajua kuwa ni muhimu na hutokana na  nyuki.



"Baadhi ya mazao kama Sumu ambayo huzalishwa kutokana na nyuki hufanya vizuri katika soko, chavua na mambo mengine ambayo hutokana na zao la nyuki." Amesema Magani.



"Ukataji wa miti umekuwa ukichangia kuondoa nyuki kutokana na kutokuwepo kwa  maua hivyo ni muhimu kutunza mazingira hayo ili kukidhi mahitaji ya nyuki" Amesema Magani.



Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Urambo amesema wamefurahishwa kushuhudia maji katika mazingira hayo hasa kuona eneo lenye maji ya moto ambayo sehemu nyingine hawajabarikiwa  kuyapata na ameshauri kukihifadhi chanzo hiki cha maji ambacho ni tunu kwa Halmashuri hii imepewa na Mungu, Pia amesema mafunzo waliyoyapata ya kufuga nyuki wangependa  yawafikie wananchi wote ambao hujishungulisha na ufugaji wa nyuki katika Halmashuri ya Urambo.



Awali Mkurungenzi Mtendaji wa Halmashuri ya Mpimbwe Bi. Catherine Mashalla ametoa shukurani kubwa kwa Baraza hilo la Madiwa na Watumishi kutoka Urambo kuja kutembelea katika Halmashuri hiI kwa ajili ya  kujifunza  swala hilo, ni swala la kuigwa hata kwa wengine.



Bi. Mashalla amesema  Halmashari hii  inajishungulisha na kilimo zaidi na hata mapato yake ya ndani hutegemea zaidi kilimo hali ambayo huchangia katika uboreshaji wa miundo mbinu yake.



Naye mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya  ya Mpimbwe Sailas Irumba amewashukuru kwa kufika katika Halmashuri hiyo na kukubali kufika kuona chanzo cha maji ya moto na kuwaomba elimu waliyoipokea waifikishe kwa wananchi wao na Halmashauri wapo tayari kupokea wageni zaidi watakaofika kutembelea na kujifunza kuhusu ufugaji nyuki na kutembelea maeneo ya vivutio kama hayo.



Imetolewa na:

Kitengo Cha Mawasiliano Serikalini

*Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe.*

Matangazo

  • BOFYA HAPA KUONA ORODHA YA WANAFUNZI WALIOPANGWA KWENDA SHULE MOJA December 20, 2023
  • TANGAZO LA KAZI YA KUJITOLEA February 15, 2024
  • Tangazo la Nafasi za Kazi September 17, 2019
  • Tangazo la nafasi za Kazi za Muda April 21, 2020
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • MPANGO WA MATUMIZI YA ARDHI HALMASHAURI YA WILAYA YA MPIMBWE

    April 05, 2025
  • MKURUGENZI MTENDAJI WA H/W YA MPIMBWE AZINDUA MAFUNZO YA UWEZESHAJI WANAWAKE KIUCHUMI KWA WATENDAJI WA KATA NA VIJIJI

    February 12, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LA MPIMBWE LAWEKA MIKAKATI YA KUBORESHA LISHE NA MIRADI YA MAENDELEO

    February 11, 2025
  • Uandikishaji kwenye Daftari la Wapiga kura

    October 11, 2024
  • Angalia yote

Video

Vivutio Vya Watali katika Hifadhi ya Taifa Katavi
Video Zaidi

Kiungo cha Haraka

  • Chuo kikiku cha kilimo Sua cha tembelea Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe kwa ajili ya uanzishaji wa chuo cha kilimo Ndani ya Mkoa wa Katavi
  • Mpimbwe A Conservation and Development Project
  • Revenue collection dashboard for Katavi Region
  • Mkoa wa katavi

Kurasa za Karibu

  • NECTA
  • UTUMISHI
  • WIZARA YA ELIMU, SAYANSI, TEKNOLOJIA NA MAFUNZO YA UFUNDI
  • OR-TAMISEMI
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya wilaya ya Mpimbwe- Usevya

    Sanduku la Posta: 245

    Telephone: 0625732265

    Mobile: 0625732265

    Barua Pepe: ded@mpimbwedc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Mpimbwe. Haki zote zimehifadhiwa