• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Anuani za watumishi |
Mpimbwe District Council
Mpimbwe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Maji
      • Ardhi na Mali asili
      • Kilimo , Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kazi na zima Moto
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mazingira na usafi
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • sheria
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • ufugaji wa nyuki
      • TEHAMA na Habari
      • Ugavi na ununuzi
    • Sehemu
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
  • Machapisho
    • Muongozo
    • Hatua
    • Taarifa
    • Sheria
      • sheria ndogo
    • Fomu ya Maombi
      • Mkataba
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Albamu ya Picha
    • Video
    • Mpya
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Matukio
    • Hotuba
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyopangwa

DC SANGA AFANIKIWA KUREJESHA HEKARI SABINI(70) KWA WAKULIMA WA KIJIJI CHA IKULWE KATA YA MAJIMOTO MKOANI KATAVI.*

Posted on: October 21st, 2022

Na. Odetha Salumu

Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe.


 

Mkuu wa Wilaya ya Mlele Filbarto Sanga amefanikiwa kurejesha hekari sabini (70) kwa wakulima zilizokuwa zimemilikiwa kinyume cha sheria na mkulima aliyejulikana kwa majina ya Chenge Samsoni mkazi wa kijiji cha Ikulwe Kata ya Majimoto wilaya ya Mpimbwe mkoa wa Katavi.


Akizungumza na wananchi katika ukumbi wa shule ya msingi Majimoto, Mkuu wa wilaya hiyo Mhe. Filbarto Sanga akiwa ameambatana na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Mpimbwe Bi. Catherine Mashalla, Mkuu wa Idara ya Ardhi Evaline Meray, Diwani wa kata ya Majimoto Mhe. Grace Udoba pamoja na watendaji ngazi ya Kijiji na kata hiyo amekemea tabia ya wananchi hao kujimilikisha maeneo ya serikali ya kijiji kinyume na sheria.


"Ninatoa rai kwa wananchi wangu wa eneo hilo, ni kosa kubwa kujimilikisha eneo ambalo si mali yako halali kwani kufanya hivyo kutachangia kuibuka kwa migogoro mingi ya Ardhi katika maeneo haya"


Awali, kipokea maelezo kutoka kwa wananchi wa eneo hilo, imefahamika kuwa jumla ya hekali 169 zilitengwa kwa ajiri ya malisho ya mifugo, baadae walijitomeza wananchi watano akiwemo Chenge Samsoni, Richard Mashelia, Obeid Bunzali, Emmanuel Kipozi na Bundala Lukuba wote wakiwa ni wakulima katika Kijiji hicho kutaka kuligawana eneo hilo kinyume na sheria hali ambayo haikufanikiwa.


Kwa mujibu wa maelezo ya wananchi hao wamefafanua mbele ya Mkuu wa Wilaya hiyo kuwa Serikali ya kijiji cha Ikulwe ilichukua jukumu la kuligwa eneo hilo kwa wananchi ambapo kila mwananchi aliuziwa hekari 1 kwa shilingi elfu hamsini (50,000.00) na kiasi cha shilingi elfu tano (5,000.00) ililipwa na mwananchi alienunua eneo hilo kwa ajili ya upimaji.


Malalamiko hayo yamekuja kufuatia mkulima aliejulikana kwa jina la Chenge Samson mkazi wa eneo hilo kulima jumla ya hekari sabini (70) Mali ya wakazi wa Kijiji na kata ya Majimoto.


Awali, Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe Bi. Catherine Mashalla alipokea Malalamiko kutoka kwa wananchi wa eneo hilo hali ambayo ilipelekea October 19, 2022 kufanya kikao cha utatuzi wa mgogoro huo, lakini mlalamikiwa Chenge Samson aliondoka kabla ya kikao kuanza hivyo ikamlazimu Mkurugenzi Bi Mashalla kuwataka wakulima kuendelea na shughuli za kilimo katika maeneo yao halali.


"Kwa kuwa nimemuita huyu bwana Chenge Samson na akaamua kupuuzia wito huu kikaoni nawaomba wananchi mkaendelee na shughuli za kilimo katika maeneo mliyouziwa awali pasipo kusumbuliwa na mtu yeyote" Alisema Mkurugenzi Bi. Catherine Mashalla


"Mkuu wetu wa wilaya Mhe Sanga atakuja kesho kutoa ufafanuzi ili haki yenu ipatikane" Alisema Mkurugenzi Bi. Catherine Mashalla


Mara baada ya Mkuu wa Wilaya kusikiliza maelezo ya wananchi na kurejea maamuzi ya mkurugenzi, Mhe. Sanga akiwa kikaoni hapo  amewataka wananchi kuzingatia sheria na taratibu wakati wanapotaka kuuza ardhi yao na waepuke kuuza Ardhi holela pale mtu anapokuwa na shida.

"Ninawasihi wananchi wangu, tuepuke kuuza Ardhi yetu kiholela kila unapopata shida nyumbani kwako, ardhi ni mtaji, ardhi ni maisha na ardhi ni muhimu kwa maisha na maendeleo ya familia zenu, tuitunze na tuepuke kutengeneza migogoro ndani ya eneo hili"

Katika hatua nyingine, Mkuu wa Wilaya ya Mleme Mhe Sanga amewaagiza wakulima hao kuendelea kulima mashamba yao na endapo watazuiliwa na mtu huyo alieamua kujichukulia maeneo hayo na kuyalima kinyume cha sheria watoe taarifa kwa uongozi wa wilaya haraka ili hatua za kisheria ziweze kufuatwa.


"Wananchi, ninawaomba mkaendelee na shughuli zenu za kilimo katika maeneo yenu aliyoyalima huyo bwana Chenge Samson, asiwatishe, katika vikao vyote cha mkurugenzi na changu hayupo ni mtu wa aina gani huyu, tutachukua hatua za kinidhamu kwa yeyote atakae jaribu kuwaonea wananchi" amesema Mkuu wa Wilaya Mhe. Sanga


Ikumbukwe kuwa Mlele ni wilaya mpya katika mkoa mpya wa Katavi, ambavyo vyote vilianzishwa rasmi mnamo Machi 2012, maeneo yake yalikuwa sehemu ya wilaya ya Mpanda na makao makuu ya wilaya yako Inyonga.


Katika zoezi la sensa ya watu na makazi la mwaka 2012 idadi ya wakazi ilikuwa watu katika Wilaya hiyo ilikuwa ni watu laki mbili themanini na mbili elfu mia tano sitini na nane (282,568), wilaya ya mlele Ina jumla ya kata ishirini na nne ikiwemo kata za Ikuba, Ilela, Ilunde, Inyonga, Itenka, Kapalala, Kasansa,  Kasokola, Kibaoni,  Litapunga, Machimboni,  Magamba,  Majimoto,  Mamba, Mbede,  Mtapenda, Mwamapuli,  Nsenkwa, Nsimbo,  Sitalike, Ugala, Urwila,  Usevya na Utende.


*Mwisho*


Imetolewa na:

Kitengo cha Habari na Mawasiliano.

Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe.

Matangazo

  • BOFYA HAPA KUONA ORODHA YA WANAFUNZI WALIOPANGWA KWENDA SHULE MOJA December 20, 2023
  • TANGAZO LA KAZI YA KUJITOLEA February 15, 2024
  • Tangazo la Nafasi za Kazi September 17, 2019
  • Tangazo la nafasi za Kazi za Muda April 21, 2020
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • MPANGO WA MATUMIZI YA ARDHI HALMASHAURI YA WILAYA YA MPIMBWE

    April 05, 2025
  • MKURUGENZI MTENDAJI WA H/W YA MPIMBWE AZINDUA MAFUNZO YA UWEZESHAJI WANAWAKE KIUCHUMI KWA WATENDAJI WA KATA NA VIJIJI

    February 12, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LA MPIMBWE LAWEKA MIKAKATI YA KUBORESHA LISHE NA MIRADI YA MAENDELEO

    February 11, 2025
  • Uandikishaji kwenye Daftari la Wapiga kura

    October 11, 2024
  • Angalia yote

Video

Vivutio Vya Watali katika Hifadhi ya Taifa Katavi
Video Zaidi

Kiungo cha Haraka

  • Chuo kikiku cha kilimo Sua cha tembelea Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe kwa ajili ya uanzishaji wa chuo cha kilimo Ndani ya Mkoa wa Katavi
  • Mpimbwe A Conservation and Development Project
  • Revenue collection dashboard for Katavi Region
  • Mkoa wa katavi

Kurasa za Karibu

  • NECTA
  • UTUMISHI
  • WIZARA YA ELIMU, SAYANSI, TEKNOLOJIA NA MAFUNZO YA UFUNDI
  • OR-TAMISEMI
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya wilaya ya Mpimbwe- Usevya

    Sanduku la Posta: 245

    Telephone: 0625732265

    Mobile: 0625732265

    Barua Pepe: ded@mpimbwedc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Mpimbwe. Haki zote zimehifadhiwa