• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Anuani za watumishi |
Mpimbwe District Council
Mpimbwe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Maji
      • Ardhi na Mali asili
      • Kilimo , Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kazi na zima Moto
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mazingira na usafi
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • sheria
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • ufugaji wa nyuki
      • TEHAMA na Habari
      • Ugavi na ununuzi
    • Sehemu
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
  • Machapisho
    • Muongozo
    • Hatua
    • Taarifa
    • Sheria
      • sheria ndogo
    • Fomu ya Maombi
      • Mkataba
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Albamu ya Picha
    • Video
    • Mpya
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Matukio
    • Hotuba
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyopangwa

WANANCHI WA MAJIMOTO WANUFAIKA NA UJENZI WA KITUO CHA AFYA MPIMBWE

Posted on: December 27th, 2022




Mapema leo tarehe 27.12.2022 Mkuu wa Wilaya ya Mlele Mhe. Filbarto Sanga amezindua utoaji wa huduma ya Tiba Kituo cha Afya Majimoto kilichopo ndani ya halmashauri ya Mpimbwe kata ya Majimoto Kijiji cha Ikulwe Mkoa wa Katavi.


Kuzinduliwa kwa utoaji wa huduma ya Tiba kituoni hapo kumekuja kufuatia utekelezaji wa agizo la Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa alilotoa tarehe 14/12/2022  baada  ya jengo la wangongwa wa nje kukamilika ipasavyo kituoni hapo.


Agizo hilo limetekelezwa na Mhe. Filbarto Sanga mara baada ya kukamilisha maagizo ambayo Waziri Mkuu ambapo alihitaji yatekelezwe na kituo kuanza kufanya kazi, aidha katika ziara yake Waziri Mkuu Majaliwa alimuagiza Mkurungenzi wa halmashauri hiyo kuhakikisha vifaa vyote vinavyo hitajika vifike kwa wakati na wananchi kuanza kupata matibabu katika kituo hiki.


Akizindua utoaji wa huduma ya Tiba kituoni hapo Mhe. Sanga amesema  kituo hicho kimejengwa kwa kutumia mapato yake ya ndani ya Halmashauri hiyo ambapo kiasi cha shilingi Milioni 423,890,000.00 zimetumika kukamilisha ujenzi huo ambapo kitanufaisha wakazi wapatao 31,842.


Kwa mjibu wa mkataba wa ujenzi huo, ujenzi ulianza mnamo tarehe 19.01.2021 na ulitarajiwa  kukamilika 20.02.2023 ambapo ulihusisha ujenzi wa jengo la wagonjwa wanje, jengo la mama na mtoto, jengo  la upasuaji, jengo la maabara, jengo la kufulia na ujenzi wa vyoo matundu 7 kituoni hapo.


"Tumezindua utoaji wa huduma ya Tiba katika kituo chetu cha Afya hapa kata ya Majimoto  rasmi leo, ni matarajio yetu wananchi wote wa kata hii na maeneo jirani watanufaika na huduma bora zitakazo patikana hapa ikiwa ni za awali na za msingi lengo likiwa ni kuwapunguzia adha wananchi ya kutembea umbali mrefu kuitafuta huduma kama itakayo tolewa hapa" amesema Mhe. Sanga.


Katika hatua nyingine, Mhe. Sanga amewataka wataalamu wa Afya waliopelekwa kufanya kazi kituoni hapo, kuzingatia misingi ya  taaluma zao wakati wakutoa huduma kwa kutoa kauli nzuri kwa wangonjwa na kuhudumia pasipo kuwa na ubaguzi wa aina yoyote kwa wananchi wote.


Naye diwani wa kata ya Majimoto Grace Udoba ameishukuru serikali ya awamu ya sita chini ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwasogezea wananchi huduma ya kituo cha Afya ambayo itasaidia  kupuguza ubali mrefu waliokuwa wakiutumia wananchi wa eneo hilo wakupata huduma hiyo.


Kwa upande wake Bi. Neema Majola mkazi wa kata ya Majimoto kwaniaba ya wananchi wa eneo hilo waliohudhuria uzinduzi wa utoaji wa huduma ya Tiba katika kituo hicho cha Afya amemshukuru Mama Samia Suluhu Hassan kwa kuwakumbuka wana majimoto kwani kuletwa kwa kituo hicho kitawasaidia wanawake wajawazito kuepukana  na vifo wakati wakujifungua na pia  watapata  matibabu wakati wote na kwa urahisi.


Imetolewa na.
Kitengo cha Mawasiliano Serikalini.
Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe.


Matangazo

  • BOFYA HAPA KUONA ORODHA YA WANAFUNZI WALIOPANGWA KWENDA SHULE MOJA December 20, 2023
  • TANGAZO LA KAZI YA KUJITOLEA February 15, 2024
  • Tangazo la Nafasi za Kazi September 17, 2019
  • Tangazo la nafasi za Kazi za Muda April 21, 2020
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • MPANGO WA MATUMIZI YA ARDHI HALMASHAURI YA WILAYA YA MPIMBWE

    April 05, 2025
  • MKURUGENZI MTENDAJI WA H/W YA MPIMBWE AZINDUA MAFUNZO YA UWEZESHAJI WANAWAKE KIUCHUMI KWA WATENDAJI WA KATA NA VIJIJI

    February 12, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LA MPIMBWE LAWEKA MIKAKATI YA KUBORESHA LISHE NA MIRADI YA MAENDELEO

    February 11, 2025
  • Uandikishaji kwenye Daftari la Wapiga kura

    October 11, 2024
  • Angalia yote

Video

Vivutio Vya Watali katika Hifadhi ya Taifa Katavi
Video Zaidi

Kiungo cha Haraka

  • Chuo kikiku cha kilimo Sua cha tembelea Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe kwa ajili ya uanzishaji wa chuo cha kilimo Ndani ya Mkoa wa Katavi
  • Mpimbwe A Conservation and Development Project
  • Revenue collection dashboard for Katavi Region
  • Mkoa wa katavi

Kurasa za Karibu

  • NECTA
  • UTUMISHI
  • WIZARA YA ELIMU, SAYANSI, TEKNOLOJIA NA MAFUNZO YA UFUNDI
  • OR-TAMISEMI
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya wilaya ya Mpimbwe- Usevya

    Sanduku la Posta: 245

    Telephone: 0625732265

    Mobile: 0625732265

    Barua Pepe: ded@mpimbwedc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Mpimbwe. Haki zote zimehifadhiwa