Kiswahili
  • English
  • Kiswahili
    • Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Anuani za watumishi |
Mpimbwe District Council
Mpimbwe District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Muundo wa Halmashauri
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Maji
      • Ardhi na Mali asili
      • Kilimo , Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kazi na zima Moto
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mazingira na usafi
    • Kitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • sheria
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • ufugaji wa nyuki
      • TEHAMA na Habari
      • Ugavi na ununuzi
    • Sehemu
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
  • Machapisho
    • Muongozo
    • Hatua
    • Taarifa
    • Sheria
      • sheria ndogo
    • Fomu ya Maombi
      • Mkataba
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Albamu ya Picha
    • Video
    • Mpya
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Matukio
    • Hotuba
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyopangwa

Wananchi watakiwa kujifunza Fursa Sekta ya Kilimo na Utalii Mkoa wa Katavi

Posted on: October 28th, 2022

 Wananchi Mkoani Katavi wametakiwa  kutumia fursa ya maonyesho ya Wiki ya Mwanakatavi kujifunza masuala mbalimbali ya Kilimo na Utalii ili kunufaika na fursa mbalimbali zilizopo katika Sekta hizo Ili  kujikwamua Kiuchumi.

Rai hiyo imtolewa na Mkuu wa Wilaya ya Mlele Bw.Filberto Sanga kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Katavi Bi.Mwanamvua Hoza Mrindoko katika uzinduzi wa  maonyesho ya Kilimo na Utalii ikiwa ni maadhimisho ya Wiki ya Mwanakatavi ya Kilimo na Utalii iliyofanyika katika Uwanja wa Shule ya Msingi Kashato Manispaa ya Mpanda

Bw.Sanga amewahimiza Wananchi kutumia vyema manyesho hayo kujifunza fursa mbalimbali katika Sekta ya Kilimo na Utalii zinazopatikana ndani ya Mkoa wa Katavi jambo litakalosaidia kuimarisha uchumi wa Mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla.

Aidha Bw.Sanga ametoa rai kwa Taasisi za Uhifadhi wa Maliasili Mkoani Katavi kuelekeza nguvu ya ziada katika ulinzi wa Maliasili hizo ikiwemo Misitu na Wanyamapori ili kunusuru rasilimali hizo dhidi ya Wavamizi.

Amewataka Maafisa Ugani Mkoani Katavi kuhakikisha wanawasajili wakulima wote kwa kuwa lengo la zoezi hilo licha ya kufanikisha zoezi la uuzaji wa mbolea ya ruzuku pia linalenga kutambua idadi ya Wakulima wote Nchini

.Katika hatua nyingine Bw.Sanga amelitaka shirika la kuhudumia Viwanda Vidogo Nchini SIDO kujenga uwezo  kwa Wajasiriamali juu ya namna ya kukuza mitaji yao ili kujikwamua na Umasikini.

Awali Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Katavi Bw.Nehemia James katika ufunguzi wa Maonyesho ya Wiki ya Mwanakatavi ya Kilimo na Utalii amesema lengo la maonyesho hayo ni kutoa fursa kwa    Wananchi Mkoani humo kujifunza masuala mbalimbali kuhusu Kilimo na Utalii pamoja na kubaini fursa zilizopo katika Sekta hizo.

MWAISHO.

*Imeandaliwa na*

kitengo cha mawasiliano Serikalini.

*Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe.*

Matangazo

  • BOFYA HAPA KUONA ORODHA YA WANAFUNZI WALIOPANGWA KWENDA SHULE MOJA December 20, 2023
  • TANGAZO LA KAZI YA KUJITOLEA February 15, 2024
  • Tangazo la Nafasi za Kazi September 17, 2019
  • Tangazo la nafasi za Kazi za Muda April 21, 2020
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • MPANGO WA MATUMIZI YA ARDHI HALMASHAURI YA WILAYA YA MPIMBWE

    April 05, 2025
  • MKURUGENZI MTENDAJI WA H/W YA MPIMBWE AZINDUA MAFUNZO YA UWEZESHAJI WANAWAKE KIUCHUMI KWA WATENDAJI WA KATA NA VIJIJI

    February 12, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LA MPIMBWE LAWEKA MIKAKATI YA KUBORESHA LISHE NA MIRADI YA MAENDELEO

    February 11, 2025
  • Uandikishaji kwenye Daftari la Wapiga kura

    October 11, 2024
  • Angalia yote

Video

Vivutio Vya Watali katika Hifadhi ya Taifa Katavi
Video Zaidi

Kiungo cha Haraka

  • Chuo kikiku cha kilimo Sua cha tembelea Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe kwa ajili ya uanzishaji wa chuo cha kilimo Ndani ya Mkoa wa Katavi
  • Mpimbwe A Conservation and Development Project
  • Revenue collection dashboard for Katavi Region
  • Mkoa wa katavi

Kurasa za Karibu

  • NECTA
  • UTUMISHI
  • WIZARA YA ELIMU, SAYANSI, TEKNOLOJIA NA MAFUNZO YA UFUNDI
  • OR-TAMISEMI
  • Watumishi Portal
  • Tovuti ya ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya wilaya ya Mpimbwe- Usevya

    Sanduku la Posta: 245

    Telephone: 0625732265

    Mobile: 0625732265

    Barua Pepe: ded@mpimbwedc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Haki miliki @2017 Halmashauri ya wilaya ya Mpimbwe. Haki zote zimehifadhiwa